Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Mzee Joseph Butiku amesema ili uchaguzi wa Oktoba uwe huru na haki vyombo vya dola vinatakiwa kuhakikisha vinavilinda vyama vyote kwa usawa, huku akieleza kuwa lengo la uchaguzi ni kupata viongozi watakao tetea maslahi ya taifa ikiwa ni pamoja kupambana na Rushwa.