Siku ya tarehe 30 Januari 2021, aliyekuwa mwanasheria mkuu wa Zanzibar, Bwana Othman Masoud Othman, alialikwa kutoa mada kwenye warsha ya siku moja iliyoandaliwa na chama cha ACT Wazalendo visiwani Zanzibar iliyokuwa inadhamiria kuangalia fursa na changamoto za hatua ya chama chao kujiunga na serikali ya umoja wa kitaifa. Msikilize kwa umakini jinsi anavyochambuwa chimbuko, mapungufu, changamoto na fursa za serikali hiyo.